Hamkani si shwari Sudan Kusini
Serikali ya Sudan Imearifu kwamba wiki iliyopita watu arobaini na tatu waliaga dunia walipokuwa katika mapambano kwenye mji huo wa Wau, ingawa raia wanasema idadi ni kubwa kuliko inavyoelezwa.
Makabiliano hayo yanatoa taswira iliyodhahiri kwamba hali ya mani bado haijatengamaa Sudan Kusini,siku mbili kabla kulikuwa na maadhimisho ya miaka hamsini ya uhuru wa nchi hiyo kama taifa huru.
Wakati hayo yakijiri yameripotiwa mapigano mengine katika mji mkuu wa Juba ambapo magari ya kijeshi yalifunga barabara mashuhuda waliliambia shirika la habari la Reuters.
No comments