Sh1.5 bilioni za Umiseta na Umitashumta zapelekwa kwenye madawati
Wakati Tanzania ilikiendelea kusuasua katika michezo, serikali imesema
zaidi ya Sh1.5 bilioni zilizotakiwa kutumika kwa ajili ya fainali za
michuano ya wanafunzi wa shule za msingi (Umiseta) na Sekondari
(Umitashumta) zitaelekezwa kwenye utengenezaji wa madawati, baada ya
michuano hiyo kusimamishwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene alisimamisha michuano hiyo ili kufanikisha agizo la Rais John Magufuli la kuhakikisha hakuna mwanafunzi atakayekaa chini ifikapo Juni 30
Akizungumza baada ya mdahalo kuhusu namna ya kuimarisha uhusiano baina ya wawekezaji na wananchi ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi, jijini Dar es Salaam, Simbachawene amesema hakutakuwa na maana kama fedha nyingi zitatumika kwenye michezo wakati wanafunzi wanakaa chini.
“Kama michezo wameshacheza na walikuwa wanaelekea Taifa, hatujazuia isipokuwa tumesimamisha hadi pale tatizo la madawati litakapoisha,”amesema.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene alisimamisha michuano hiyo ili kufanikisha agizo la Rais John Magufuli la kuhakikisha hakuna mwanafunzi atakayekaa chini ifikapo Juni 30
Akizungumza baada ya mdahalo kuhusu namna ya kuimarisha uhusiano baina ya wawekezaji na wananchi ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi, jijini Dar es Salaam, Simbachawene amesema hakutakuwa na maana kama fedha nyingi zitatumika kwenye michezo wakati wanafunzi wanakaa chini.
“Kama michezo wameshacheza na walikuwa wanaelekea Taifa, hatujazuia isipokuwa tumesimamisha hadi pale tatizo la madawati litakapoisha,”amesema.
No comments